UNAFANYA NINI USIKU WA MANANE??
Matendo 16:25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Unaposikia neno usiku wa manane unaelewa nini???
Kwa tafsiri rahisi usiku wa manane ni masaa ya usiku yaanzayo saa 6 hadi 8 au 9 ndiyo kwa lugha rahisi hujulikana kama usiku wa maneno. Kwa kawaida masaa haya ni masaa ya pekee sana katika historia ya siku. Katika sehemu nyingi duniani masaa ya usiku wa manane ni masaa ambayo kwayo watu wote wamelala ikiwa ni vijijini kijiji kizima kinakuwa kimya masaa haya maana shughuli zote zimesimama. Kwa maeneo ya mjini masaa haya pia dunia huwa kimya na hata kama kuna shughuli za kimaendeleo zinafanyika basi ni chache sana na huenda kwa sehemu chache pia.
Usiku wa manane ni masaa ambayo kwa asilimia kubwa dunia inakuwa imetulia kimya maana shughulu nyingi zimesimama, usiku wa manane ni masaa ambayo kuna giza nene pasipo mwanga hata mdogo huwezi kutembea hata hatua moja. usiku wa manane ni nyakati ambazo kwazo shughuli nyingi za kiualifu hufanyika maana watu wanakuwa wamelala wasijue chochote kinachoendelea huko nje. Usiku wa manane ni masaa ambayo mtu haoni mbele nyuma wala pembeni kwa kuwa kote kumetanda giza na hakuna mwanga. Ni nyakati ambazo hata ukikutana na mtu kumwamini inakuwa shida maana hujui kusudi lake katika nyakati hizo ni nini zaidi sana utamdhania kuwa si mtu mwema.
Usiku wa manane unafanya nini????
Kisa cha Paulo na Sila kinaanza katika matendo ya mitume sura ya 15 wakiwa Antiokia matendo 14:26 Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza. katika shughuli zao za uinjilisti mara baada ya Paulo kuongoka.katika sura ya 15:1 Wakashuka watu waliotoka Uyahudi wakawafundisha wale ndugu ya kwamba, Msipotahiriwa kama desturi ya Musa hamwezi kuokoka. Kwa sababu ya mjadala wa kidini juu ya kutahiriwa au kutokutahiriwa kwa wale wamataifa walioongoka wapya kama torati ya Musa ilivyoamuru walishindwa kufikia muafaka kwa sababu wapo walisema ni lazima kutahiriwa na waliosema si lazima kutahiriwa.
Kwa sababu ya mabishano hayo Paulo na Barnaba waliamua kupanda kwenda Yerusalemu kuwauliza wazee wa baraza na baadhi ya mitume waliokuwepo hapo akiwemo na Petro Matendo ya mitume 15:2 Basi baada ya Paulo na Barnaba kushindana na watu hawa na kuhojiana nao sana, ndugu wakaamuru kwamba Paulo na Barnaba na wengine miongoni mwao wapande kwenda Yerusalemu kwa mitume na wazee kwa habari ya swali hilo. Baada ya mahojiano katika baraza na Petro kutoa hitimisho (matendo 15:7-11) Paulo na Barnaba wanarejea Antiokia na uhjumbe waliopewa. Na ndipo walipohitaji kurejea katika hiyo miji waliowahi kupeleka injili ili kuwajulia hali hao waongofu. Barnaba anamchukua marko (yohana), na Paulo anamchukua Sila (fungu la 36-41)
Wakipita katika miji kama Derbe, Listra, ikonio, firgia na Galatia kote huku walikuwa wakihubiri habari njema wakapita Misia wakatokea Troa. (Matendo 16:1-8). Ndipo Paulo anazuiliwa na Malaika asihubiri katika Asia lakini matendo 16:8 Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. Ndipo
Fungu la 8 Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie. Hata ilipofika sabato walitafuta kanisa ili wasali matendo ya mitume 16:13 Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale. Mmojawapo wa wanawake hao alikuwepo mwanamke aliyeitwa Lidia.
Tukio la ajabu na la pekee linaliokumba safari ya Paulo na sila huku Makedonia ni kukutana na binti kijakazi aliyekuwa na pepo wa uaguzi aliyewapatia bwana zake faida kwa kuagua matendo ya mitume 16:16 Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua. (kuagua ni nini??) paulo alisikitishwa sana na kitendo cha yule binti kupiga kelele mara kwa mara na hivyo alimuamuru yule pepo kumtoka yule binti nayo pepo ikamtoka saa ile ile matendo ya mitume 16:18 Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.
Binti huyu alikuwa ni chanzo zha mapato kwa bwana zake maana kwa kitendo cha uaguzi aliwapatia faida. Kitendo cha Paulo kumtoa pepo kilizua tafrani maana bwana zake waliona sasa wamepoteza chanzo cha mapato. Waliwakamata Paulo na Sila na kuwapeleka sokoni mbele za wakuu wa mji matendo ya mitume 16:19 Basi bwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limewapotea, wakawakamata Paulo na Sila, wakawakokota mpaka sokoni mbele ya wakuu wa mji; usicheze na chanzo cha mapato cha mtu hasa wakubwa!! waliadhibiwa na kuchapwa kwa bakora na kasha kuamriwa kutupwa gerezani na kufungwa na mkatale matendo ya mitume 16:23,24 Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana.Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale. (mkatale ni ubao uliotobolewa unaingizwa miguuni na kufungwa kwa kufuli)
Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwimba Bwana na kumwimbia nyimbo za kumsifu na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Matendo ya mitume 16:25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza. Katika hali isiyo ya kawaida si rahisi kuwakuta mahabusu au hata wafungwa wakiwa ndani ya cello (korokoroni, kifungoni) wakifanya hata ibada, mara nyingi wengi wakishafika kule hupoteza tumaini na kuona kama ndio mwisho wa maisha yao hata kama ulipelekwa kwa kusingiziwa ama kuonewa. Na ukifika katika gereza huwezi kusikia hata sauti ya mtu ikiimba nyimbo za Kristo zaidi sana ataimba nyimbo za kiduni (jela ni mbaya jela ni amteso). Lakini hapa tunakutana na wafungwa wawili jasiri ambao pamoja na kupigwa kwingi na kufungwa na mikatale bado hawakujali maumivu wala uchovu waliokuwa nao (maana huenda kwa sababu ya maumivu ya viboko na mkatale wangeamua kulala zao wakisubiri adhabu ambayo ingewakabili kesho yake) lakini watu hawa wanamuomba Mungu na kumuimbia nyimbo za kumtukuza
Matokeo ya maombi na nyimbo hizi ni tetemeko kubwa katika nchi yote na misingi ya gereza ikatikisika vifungo vyote vikalegea matendo ya mitume 16:26 Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa. Ni kwa nguvu ya maombi na nyimbo milango ya gereza ikafunguka mlinzi aliogopa hata kutaka kujiua lakini paulo alimsihi asijiue maana hawajatoroka lakini kubwa zaidi waliamuriwa watolewe gerezani maana wakuu wa mji waliogopa kwa tukio lile.
unafanya nini usiku wa manane??
Usiku wa manane kwako ni nini? Ni changamoto gani unayoipitia katika maisha yako? Ni jambo gani kubwa kwako linalokuzinga hata usimuone Kristo sasa? Giza lipi limekufunga hata huoni nuru tena, ukiangalia mbele ni giza nyuma giza pembeni giza? Tumaini lako liko wapi wakati wa giza nene lililokuzingira pande zote?
Huenda usiku wa manane kwako ni ugonjwa, umeugua kwa muda mrefu sasa na huoni tena tumaini katika maisha yako ukidhani ndio mwisho wako… huenda usiku wa manane kwako ni changamoto za ndoa au mahusiano ya uchumba na sasa unalia kila siku huoni tumaini tena, huenda usiku wa manane kwako ni ajira na shughuli zako za kiuchumi zinazokuwia ugumu kila siku na sasa unapoteza tumaini… huenda usiku wa manane kwako ni changamoto ya kiimani unayoipitia katikati ya ndugu zako jamaa au hata rafiki, unafukuzwa kazi kila siku kwa sababu ya imani nawe huoni tena tumaini… umefungwa na nini? Paulo na sila walifungwa na mkatale……
Kumbuka ni katika usiku wa manane imetupasa kumuita Kristo kuliko nyakati zote tumewahi kumuita. Ni katika usiku wa manane imetupasa kumuomba Mungu na kumuimbia nyimbo za sifa hata wafungwa wengine wasikie.. ni kwa maombi na nyimbo tetemeko kuu litasikika katika nchi navyo vyanzo vya usiku wa manane kwako vitaogopa. Kama ni ndugu jamaa marafiki au waajiri wako wataogopa na kukupa uhuru wako, kama ni njaa misiba vita nk nk vitakimbia maana Bwana atajifunua kwako sasa. Maombi na nyimbo hutikisa misingi ya muovu
USIKU WA MANANE OMBA NA KUMUIMBIA MUNGU NYIMBO ZA SIFA
BWANA AWABARIKI
BY Pierre de' Jefter
0783167164
peterjefter91@gmail.com
Hello There. I found your blog using msn. This iis a very
ReplyDeletewell written article. I will make sure to bookmark it
and return to read more of your useful information. Thanks for the post.
I willl certainly comeback.